Ngara: Mbunge Abanwa Koo Kulipa Mishahara ya Katibu Saa 9 Usiku

By admin May 3, 2025
Pesa ni kila kitu. Wanasema pesa ni sabuni ya roho. Minong'ono ni mingi Wilayani Ngara juu ya Mbunge wa jimbo hilo kutolipa ahadi. Kuna wengine wanasema wanamdai milioni kadhaa kwani kuna kesi za kizushi wilayani Ngara ambapo wasaidizi wake walilazimika kujigusha mfukoni ili walipe gharama za mahakamani ili kumstili mwanasiasa aliyekua nyuma ya hizo kesi. Kesi ziliposhindikana kuleta matunda, mwanasheria aliyejigusa mfukoni kulipa gharama za mahakama na wapambe waliojitwisha msalaba wa kutumika kama wafungua kesi, basi hela iliishia kwenye ahadi tu. Wasaidizi wa Mbunge wengi wameshamkimbia kwani jamaa anayajenga tuu kwa kinywa ila simulizi zake haziwezi perekwa dukani na kununua unga ili watoto na familia ile. Sasa hadi katibu alitingisha kibiliti kwa kudai anajihudhuru kama mishahara ya miezi mitatu haitolipwa. Kwa njia ya simu, mishahara ya miezi mitatu yote ilipokelewa na katibu akaonekana amebadilisha kauli; akadai hajihudhuru tena kwani alikua anaangalia kama Mbunge alikua na maadui wengi. Maadui akimanisha alikua kakaukiwa hela na madeni yanamsongoma. Pesa ndio inafanya dunia izunguke; hamna uzalendo bila pesa, hamna usaidizi bila pesa. Hata maswala ya mipango ya kesi za ajabu sasa inaanza kuvuja kwani hata kule mahakamani gharama zisingelipwa kana utu uzima na busara zisingetumika. Lipa pesa jamani ili usivuliwe nguo; mbona unazitafuta sana huko machimboni? Pesa sio ya kuhifadhi na kukumbatia, pesa ni ya kutumia ili huduma isisitishwe. Ukatibu hautositishwa ila kwa miezi iliyobakia usidai muda umeisha na ukapuuzia kulipa mshahara kwa wale wanaosaidia kazi zako.

Kumbe Kinachowakimbiza Wasaidizi wa Mbunge Ni Mishahara!

Nikipiga stori na mchizi wangu mmoja pale Kenga anasema si takwa la kisheria kwa Mbunge kulipa moja kwa moja wahudumu wake binafsi kama katibu, msaidizi wa ofisi au dereva.  Kwamba Katika mfumo wa kisheria na kiutawala nchini Kenya ,watu kama  wahudumu wa Mbunge walioko katika ofisi ya bunge au walioteuliwa rasmi kupitia Bunge hulipwa na Serikali kupitia mfuko wa Bunge, si na Mbunge binafsi.

Sasa kweru ni tofauti. Wote walioko Ofisini kwake tumeajiriwa ndiyomaana anaguchukukia poa tu……(Jina kapuni).

Juzi moja ya group ya Ngara kuliwaka ðŸ”¥ ðŸ”¥ ðŸ”¥ ðŸ”¥baada ya katibu wa mzee Ndayisaba Ruholo kutimiza miezi kadhaa bika kumlipa katibu wake Mr. Ruhubu Enest!  Moto ulipokolea saa 9 usiku Mheshimiwa akamsongeshea mshiko kwa simu,weeeee!

Stori ni nyibgi kwa boss kutolipa watumishi wake ofisini na kiwanda. …..mbona wengi walitema mzigo na kukimbia? (Swahiba wake).

Madereva,katibu,mlinzi wote walitembea!!!

Wakati mwmbo yanakuwa ya ðŸ”¥ ðŸ”¥ ðŸ”¥, profesa mmoja akaandika hivi……..

Watu 6 waliong’atwa na kupulizwa hapo hapo na Ruhoro halafu !

1.Conrad na wenzake~hawa walimuimba vibaya akawashughulikia

2.Manyaga~Alinyimwa maslahi yake aliyokuwa akimdai baada ya kumwanika mitandaoni akalipwa maslahi yake yote.

3.Josias Charles ~Alinyimwa posho ya milioni 1 kutoka kwake ilihali alikuwa kamuahidi hela ikitoka atampatia,hela ilivyotoka ikaelekezwa mgodini,Josias akasema usinitanie naondoka

4.Juventus Juvinary~huyu alikuwa Katibu wa Mbunge,inasemekana aliingia kwenye hii nafasi na shauku kubwa ya kuvuna mafanikio lakini aliondoka kama alivyoingia

5.Selemani Bunzia~Huyu alipewa laki 5 ya kununua vigae baada ya kuzingua akaanikwa kwa slip ya CRDB kwenye magroup yote.

6.Huyu ni ERNEST RUHUGU,katibu wa mbunge ambaye see more….!

Tusubili na kuona

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *