PIKIPIKI 57 ZILIZOPASWA KUGAWIWA KWA VIKUNDI 6 VYA VIJANA NGARA KUPITIA 10% ZIKO WAPI? NYUMBANI KWA MBUNGE?
Na: Josias Charles
Siku kadhaa zilizopita nilidokezwa na moja ya wananchi wa Wilaya ya Ngara kuhusu jambo lisilo la kawaida ambapo inadaiwa kuwa Pikipiki takribani 57 zilizotolewa kwa Vikundi 6 vya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara zimehifadhiwa Nyumbani kwa Mbunge kwa kile kinacho onekana kama mpango mahususi wa “Drama” ya Mbunge kugawa pikipiki hizo kama sehemu ya Kujiimarisha kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao.

Jambo hili lilinisikitisha sana ukizingatia kuwa Wenye Jukumu la Kutoa Mikopo ya 10% Mapato ya Halmashsuri ni Serikali Kupitia ma Afisa wa Halmashauri na sio suala la Mwanasiasa yoyote kuuteka mchakato huo.
Lakini pia Mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya
ndani ya Halmashauri kwa vijana
wanawake na watu wenye ulemavu
inafanya kazi kama mfuko unaozunguka
ambapo Kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ya Serikali za
Mitaa (Sura ya 290, Kifungu cha 37a)
inazielekeza Halmashauri zote kutenga
asilimia 10 ya mapato yake ya kila
mwaka kwa ajili ya kutoa mikopo isiyo
na riba kwa vikundi vya wanawake
(4%), vijana (4%) na watu wenye
ulemavu (2%). Mikopo hii inakusudiwa
kuimarisha shughuli zinazowaingizia
kipato wanawake, vijana na watu wenye
ulemavu wasio na ajira rasmi na hivyo
kuboresha maisha yao kwa ujumla.

Nyenzo za kusafiri kwa watu wengi zimerahisisha maisha na kutoa fursa kwa wengi, hususani vijana. Piki piki, maarufu kama boda boda, zinatumiwa na serikali kutengeneza ajira. Boda boda pia zinaleta changamoto kama uvunjifu wa sheria za bara barani (traffic). Pia, ajari mbali mbali ambazo zinafupisha maisha ya watu wengi na kuonyesha udhaifu wa huduma za afya zilizopo hapa Tanzania kwani ajari zinazotokana na matumizi ya boda boda zinalazimisha viongozi kufikiria na kuboresha huduma zilizopo mahospitalini.
Hivyo basi, Suala la Pikipiki 57% za Halmashauri kuhifadhiwa kinyume na utaratibu nyumbani kwa Mbunge linalenga kuzorotesha lengo mama la Kutolewa kwa mikopo hiyo kwani Pikipiki hizo zilistahili kuwa kwenye shughuli za uzalishaji mali ili kuimarisha kipato cha Vijana na pia kusaidia Vijana waliokopeshwa kurejesha mikopo kwa wakati na hatimaye kutoa fursa kwa vijana wengine kukopeshwa.
Kwa andiko hili, ninatarajia kuona Ofisi ya Mbunge ikijitokeza hadharani na kufafanua kinagaubaga kuhusu sababu hasa ya Kuhifadhi pikipiki hizo 57 kwenye makazi binafsi ya Mbunge na ni kwa namna gani Ofisi ya Mbunge inahusika na Mchakato wa upatikanaji na ugawaji wa Pikipiki hizo.

Lakini pia ni matumaini yangu kuwa Ofisi zinazo husika na utoaji mikopo katika ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara zitatoka hadharani na kuelezea ni kitu gani haswa kinaendelea hivi sasa kuhusiana na Pikipiki hizo na ni sababu zipi zimepelekea pikipiki hizo 57 kuwa katika makazi ya Mbunge badala ya kuwafikia walengwa ambao ni Vikundi 6 vilivyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara.

Piki piki ambazo ilikua ziende kwa vijana zimehifadhiwa nyumbani kwa Mhe Ruhoro.
Kama mdau wa maendeleo katika Wilaya ya Ngara nina tahadharisha kuhusu athari za Kuleta siasa kwenye masuala yanayohitaji Uwajibikaji na Sheria. Ninaamini kama mchakato huu wa Utoaji mikopo ya 10% utaingiza siasa utasababisha wakopaji kutokulipa mikopo hiyo na hivyo kuathiri vijana wengine ambao walitarajia kukopa.
