John William Ndenzako, ni mkazi wa Kabanga wilayani Ngara ambaye hajabahatika kuwasiliana na binti yake aitwae Josephine John. Josephine John alizaliwa mwaka 1980 kwa familia ya Venance Nzeye wa Munanila, Manyovu, Tanzania. Josephine anatafutwa na baba yake.
Mzee Ndenzako ametembelea gazeti hili na kuomba asaidiwe kufikisha habari kwa jamii ya kwamba anamtafuta mtoto wake pekee. Mara ya mwisho walipotezana mwaka 1985 huko Urambo Tabora. Tafadhali sambaza hii link katika majukwa mbali mbali na kwenye facebook ama anayemfahamu ama anayejua alipo Josephine awasiliane na mzee John William Ndenzako kwa simu namba 078-617-0071.