Tarehe 29, mwezi wa Sita ni siku ambayo Mwalimu Frank Peterson Aliagana na Ukapera,.
Hongera Sana Mwalimu Frank
Kwa niaba ya timu ya Walimu, ndugu jamaa na marafiki wa Mkurugenzi wa Ngara TV tunaungana na watu wote waliotushika mkono kuhakikisha kijana wetu anafunga ndoa.
Imekua Rasmi: Chombo ya Mkurugenzi wa NgaraTV, Ndugu Frank P Mshenyera: Hahitaji kujipodoa, uzuri wake tuu wa Natural ni bomba mbaya. Hongera sana Mwalimu wetu.
Tunamtakia maisha mema yenye Utulivu maana Mwalimu ni kioo cha jamii.
Mwalimu shemeji pia amtunze Mme wake sawasawa na mapenzi ya Mungu.
Tulisafiri salama, na kurudi vizuri
Mwalimu Frank: Kwa Unyenyekuvu na shukrani kwa Mungu na Mheshimiwa mwenyewe nawashukuru kwa yote kwani nimeishi na nikakamilisha harusi yangu. Ni bahati kubwa kuwa na kifaa kama hii. Nashukuru pia nyote na hasa walimu wenzangu kwa kuhakikisha mambo yametimia kama yalivyokua yameandaliwa. Picha na Kamera Nene wa Simamiatv.
Mrembo nimekuchagua wewe uwe ubavu wangu uliokuwa umesalia. Na amaini Mwenyezi Mungu ataendelea kutubariki na hata tulete matunda mema ambayo yatakua na faida nyingi kwa dunia hii.
Kwa kufikia siku ya leo na kwa kukamilisha shughuli nzima, nawashukuru kwa michango yenu, upendo wenu na kwa kunipokea ili niwe sehemu ya familia yenu hapa Ngara na Mungu awazidishie mlipotoa.