Bodaboda Wanatumika Kisiasa

By admin Mar 23, 2024
Boda Boda ni biashara na wito ni kutoa huduma kwa mteja wao. Mteja anaweza kuwa mchungaji, shekhe, mwanasiasa, ama kahaba. Nia ya kuhitaji usafiri si hitaji la msafirishaji kwani boda boda kazi yake ni kutoa huduma na kumfanya mteja ajihisi ni malikia. Je, bei ya huduma ipande pale boda boda hudumia wanasiasa?

Kuliwahi kuwa na malumbano ya baadhi ya wanasiasa na viongozi kuhusu Bodaboda kuwa ni kazi au lah!

Nakumbuka, malumbano yalichukua takribani siku kadhaa; baadhi wakiitetea kuwa ni kazi inayowaingizia kipato vijana huku wengine wakiita laana.

Wengine walienda mbali wakauita ubodaboda kama kazi ambayo ni kichaka cha baadhi ya makundi ya wahalifu kwani huhusika na kusafirisha wahalifu, na wakati mwingine baadhi ya waendesha bodaboda wenyewe kushiriki katika kufanya uhalifu.

Wapo baadhi ya bodaboda waliofanikiwa kupata maendeleo kupitia kazi hiyo na kuweza kujenga nyumba, kuanzisha Miradi na hata kusomesha watoto shule za maana. 

Lawama za bodaboda kwa jamii ni pale wanapohusishwa na mambo yanayohatarisha usalama wa raia kama vile kusafirisha wezi, kubeba wasichana wa shule au kujihusisha na mapenzi kwa wanafunzi na hata wake za watu.

Hivi karibuni, imebainika mchezo wa kisiasa ambao unawanasa bodaboda wa Wilaya ya Ngara katika harakati za baadhi ya Wanasiasa.

Mbunge wa Jimbo la Ngara George Ndaisaba Ruhoro ni mmoja wa watu wanaowaingiza bodaboda  kwenye mtego huo kwa kuwatumia kupata Umaarufu.

“Mara nyingi sana anawatumia watu wake kutuita kama ana mikutano” alisema bodaboda mmoja aliyejulika kwa jina la Rama.

Mwingine aliyezungumza bila kutajwa jina lake, alisema “Sasa kama anatuwekea mafuta, na akatupiga posho ya elfu 10 kwanini tusimsinfikize?”

Imebainika kuwa Mbunge huyo wa Ngara, kupitia kwa mratibu wa shughuli zake na wapambe wengine  humpangia ratiba za mikutano kwa kumpatia bajeti inayohusisha mafuta na posho za bodaboda ambao hupamba misafara yake kwa maandamano.

Mabadiliko yanapotokea siku zote huja na changamoto na penigne kuja na faida mbali mbali. Jamii hunufaika pale uzito wa mafanikio unapozidi ule wa changamoto. Na uwepo wa boda boda, pengine na uwepo wa teknologia isiyokwepeka ambayo imewezesha utandawazi kuchochea utamu wa maisha ya ulimwengu wa leo, kero ya kufikisha wagonja kwenye vituo vya afya imepungua. Mawasiliano yameongezeka kati ya jamii moja hadi nyingine kwani uwepo wa njia za usafiri, watu wanaweza kutembeleana. Uwepo wa madiliko ya nyenzo zinazorahisisha mawasiliano umechangia katika ubora wa maisha ya leo. Ila changamoto ni pale wanasiasa wanapojaribu kujitajirisha kwa kusaka vyeo huku wakiwalalia na muda mwingine kuwazulumu waendesha maboda boda. Pengine vyama vinavyojihusisha na uongozi wa soko la boda boda uweke msimamo mmoja ili kuokoa unyanyasaji unafanywa na wanasiasa kwa kuburuza waendesha boda boda na kwa kutumia mafuta kama hongo. Anayetoa ama kupokea hongo ni mvunjifu wa sheria. Pale hongo inapotolewa na kiongozi, unyanyasaji kwa yule ambaye si kiongozi hutokea na nikipindi cha kutetea na kulinda usawa kwani wanaoendesha hizi boda boda wana ndugu na familia zinazotegemea chochote kinachopatikana huko makazini.

Aidha, hali hiyo pia inatoa fursa za upigaji kwa baadhi ya waratibu ambao hupata viwango wanavyotakiwa kulipwa Bodaboda na kuwapa malipo pungufu.

“Siamini kama tunacholipwa ndicho kinatoka kwa Mheshimiwa, kwasababu hatujawahi kuzidishiwa Lita 2 labda siku moja-moja huku Rulenge ndio anatoa mpaka  elfu 10.” Alisema bodaboda alliefahamika kama Sinzo.

Kwa ushuhuda wa bodaboda hao wakizungumzia mikutano ya Mbunge ni kweli wanatumika. 

Ushauri wetu, wasikatae kufanya kazi zinazowaingizia kipato. Ila, wachukue tahadhali.  Wakumbuke  Wanasiasa wanakuja na kuondoka. Muda wao ukiisha, hawatawakumbuka.

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *