Mbunge Ndiye Anayesaidia ama Serikali?

By admin Mar 8, 2024
Kati ya Serikali, Chama, ama Bunge, lipi linaleta misaada kwa wananchi?

Nafasi ya Mbunge ni Ipi katika Hili, na Serikali Je?

Iko wapi nafasi ya Serikali na Chama Tawala?

Wananchi wengi wenye uelewa wao waliosoma tangazo hili naumebakia na maswali mengi.

TANGAZO KWA WASTAFU WOTE NGARA

Mbunge wa Jimbo la Ngara MH *NDAISABA G RUHORO* anapenda kuwatangazia wastafu wote kuwa, amefanikiwa kuwaomba PSSSF kuja kufanyia uhakiki wa WASTAFU NGARA kwa Mara nyingine tena.

Uhakiki utafanyika siku ya jumanne 12.03.2024 pale Halmashauri ya Wilaya ya Ngara  kuanzia saa tatu na nusu asubuhi. 

Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mbunge atakuwepo ili kusaidia zoezi zima la Uhakiki wa Wazee wetu wastaafu.

Mstafu atakae pitwa na uhakiki huu atalazimika kwenda Bukoba kupata huduma hii.

Upatapo taarifa hii Mjulishe na Mwenzako.

Wenu

Ernest Benedicto

Katibu wa Mbunge.

Tumtumie maoni yako kwa kuacha maoni hapa chini. Kubaki kimya pia ni busara njema tuu.

By admin

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *